Mguu wa Kurt Zouma ulivyopinda mara baada ya kutua vibaya alipokuwa ameruka juu.
Beki wa
kati wa Chelsea, Kurt Zouma ameumia goti lake upande wa nyuma baada ya
kutua vibaya wakati akirejea chini alipokuwa akiwania mpira wa juu
katika mechi dhidi ya Man United iliyoisha kwa sare ya bao 1-1.
Beki huyo anaweza akakaa nje ya uwanja kwa muda mrefu na tayari wachhezaji wengine wakianza wa Man United, wamekuwa wakimliwaza.
…Akilia kwa uchungu baada ya kuumia
Juan
Mata, alimfuata palepale uwanjani na Marouane Fellaini alikuwa wa kwanza
kumpa pole baada ya mechi kwisha, lakini beki Luke Shaw ambaye pia ni
majeruhi pia alitupia mtandaoni akimuombea apone haraka.
…Akitoka nje ya uwanja
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269