Kutoka
kushoto Mratibu wa matukio wa King Solomon Events, Bi Hellen Kazimoto,
Ben Pol, Patricia Hillary na muwakilishi wa Mgahawa wa Eaters Point Chef
Sub
Pete
iliyotengenezwa kwa madini ya Tanzanite yenye thamani ya shilingi za
kitanzania Milioni nne, huenda ikawa mali ya wapendanao watakaokuwa na
bahati, maana ni miongoni mwa zawadi nono zitakazotolewa katika onesho
la wapendanao lililopachikwa jina la Valentine Affair linalotarajiwa
kufanyika katika ukumbi wa King Solomon jijini Darv Salaam katika siku
ya Wapendanao Jumapili hii.
Akiongea
na wanahabarti, Mratibu wa Matukio wa kampuni ya King Solomon Events, Bi
Hellen Kazimoto amesema Kampuni hiyo inayokuja kwa kasi katika mambo ya
burudani, baada ya kukonga nyoyo za mashabiki kwa matamasha yake
yaliyoonesha mapinduzi katika sekta ya burudani nchini, yakiwemo ya
Party in The Parking na ziara ya mwanamuziki WizKid jijini Dar es
salaam, sasa wanakuja na tamasha jingine kubwa zuri na la kusisimua
katika msimu huu wa wapendanao.
Tamasha
limepewa jina la Valentine Affairs ambapo litawapa nafasi wapenda
burudani na wapendanao kwa ujumla kujumuika pamoja kwa ajili ya chakula
chenye hadhi ya nyota tano na muziki wa kutumia ala utakaoshirikisha
wanamuziki mahiri wa miondoko laini nchini, wakati huo huo zawadi za
aina yake zikitolewa ukumbini hapo.
Onesho
hilo litakalofanyika katika ukumbi wa King Solomons, Jumapili ya Tarehe
14 Februari, 2016, kuanzia saa 12 jioni na kuendelea linatarajiwa
kupambwa na wanamuziki BenPol, Grace Matata pamoja na mkongwe Patricia
Hillary.
Wanamuziki
hawa watakuwa wakipigiwa muziki maalum kwa ajili ya wapendanao kwa
vyombo vya ala, na watakuwa wakiburudisha wapendanao muda wote
watakapokuwa katika eneo la tukio kuanzia kuwasili kwao, mpaka muda wa
chakula n ahata wakati wa kupeana zawadi.
Zawadi
zitakazotolewa ni pamoja na pete kwa wapendanao watakaokuwa na bahati,
ni Pete yenye thamani ya shilingi Milioni nne, iliyotengenezwa kwa
madini ya tanzanite, kutoka Gift Jewelers. Zawadi nyingine ni malazi ya
siku mbili kwa wapendanao katika Hoteli ya Regency Park Hotel ambao pia
ni wadhamini wa onesho hilo la aina yake ya wapendanao.
Zawadi
nyingine ni vocha yenye thamani ya shilingi laki mbili za kitanzania
kutoka kampuni ya King Solomons ambayo inaweza kutumika katika mgahawa
wa Eaters Point au Wantashi.
Usiku huu
wa Valentine Affair umefanikishwa na wadau mbali mbali kwa kushirikiana
na King Solomons Events ambao ni Wantashi, Coca Cola, Eaters Point,
EATV, EA Radio, Regency Park Hotel, Gift Jewelers pamoja na twenty4
Printers.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269