Breaking News

Your Ad Spot

Feb 8, 2016

TAMKO LA WAZIRI UMMY MWALIMU KUHUSU UGONJWA WA KIPINDUPINDU

UM2
TAMKO KUHUSU MWENENDO WA UGONJWA WA KIPINDUPINDU NCHINI PAMOJA NA TAHADHARI YA UGONJWA WA HOMA YA ZIKA, LILILOTOLEWA NA MHE. UMMY MWALIMU (MB); WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO Y
A JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO, TAREHE 8 FEBRUARI 2016.
…………………………………………………………………………………………..
Kuhusu ugonjwa wa kipindupindu, huu ni mwendelezo wa taarifa ya wiki kwa umma, ya mwenendo wa ugonjwa huu hapa nchini. Hadi kufikia tarehe 7 Februari 2016, jumla ya watu 15325 wameugua ugonjwa huo, na kati yao watu  238 wamepoteza maisha kwa ugonjwa huu.  
Takwimu za Kuanzia tarehe 1 hadi 7 Februari 2016, zinaonyesha kuwa idadi ya wagonjwa walioripotiwa wiki hii imepungua kutoka 459 ya wiki iliyoishia tarehe 31 Januari hadi 258 ambapo ni sawa na punguzo la asilimia 44. Kuna vifo 5, sawa na idadi ya vifo vilivyoripotiwa katika wiki iliyopita.
Jumla ya mikoa ambayo imeripoti kuwa na wagonjwa ni 13 ambapo mkoa wa  Mara ndio umeongoza kwa kuripoti idadi kubwa zaidi ya wagonjwa ukilinganishwa na mikoa mingine, ukiwa na wagonjwa 73 (Musoma Vijijini 33,  Musoma mjini 5, Bunda 1, Butiama 13, na Tarime Vijijini 21), ukifuatiwa na mkoa wa Mwanza (70)- (Ukerewe 21, Nyamagana 24, Ilemela 8, Sengerema 5 na Buchosa 12). Mikoa mingine ni pamoja na Simiyu (30), Morogoro (26) na Kilimanjaro (16). 
Katika mapambano ya kudhibiti mlipuko huu wa Kipindupindu, kuna changamoto mbalimbali zilizobainishwa na Wizara yangu kupitia wataalam ambao wanashirikiana na timu zilizopo katika mikoa na wilaya zilizoathirika. Mojawapo wa changamoto ni utoaji wa idadi pungufu ya wagonjwa au kutotoa kabisa taarifa za wagonjwa wa Kipindupindu. Hii inapelekea kusababisha mikakati iliyowekwa kutokuwa na mafanikio hivyo ugonjwa kuendelea kuwa ni tishio katika jamii. Ninapenda kusisitiza kuwa, taarifa za wagonjwa wa Kipindupindu zitolewe bila kuficha, na watendaji watakaoficha taarifa za wagonjwa watawajibishwa ipasavyo.
Changamoto nyingine iliyopo ni ushiriki mdogo wa sekta nyingine katika kupambana na ugonjwa huu. Ninaomba ieleweke kuwa mapambano dhidi ya Kipindupindu yatafanikiwa ikiwa sekta nyingine kama Maji, miundombinu, biashara, elimu, mazingira n.k zitashirikiana. Wizara yangu imeendelea kusisitiiza ushirikiano huu katika ngazi ya Taifa, Mkoa na Wilaya, ili mipango ya kupambana na Kipindupindu ishirikishe sekta mbalimbali na pia Mashirika yasiyo ya Kiserikali, Taasisi za Dini na Vyombo ya Habari

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages