Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Michezo
Zanzibar BMZ akizungumza wakati wa hafla hiyo ya kukabidhi fedha kwa
timu za JKU na Mafunzo za mchezo wao wa Kombe la CAF inayotarajiwa
kufanyika katika Uwanja wa Amaan Zanzibar.
Meneja wa Makampuni ya Hoteli za Ocean
View, Zanzibar Jacob Makundi akizungumza na Waandishi wa habari na
Viongozi na Wachezaji wa Timu za JKU na Mafunzo (hawapo pichani) wakati wa kukabidhi
fedha za ununuzi wa tiketi wa michuano hiyo inayoandaliwa na CAF
Championc Leagua na Confederation Cup 2016. na kuahidi kutowa gharama
zote za michezo hiyo. inayotarajiwa kufanyika feb 13 na
14 mwaka huu katika uwanja wa amaan Zanzibar.
Viongozi wa Timu za JKU na Mafunzo
wakimsikiliza Meneja wa Makampuni ya Zanzibar Ocean View Zanzibar
akizungumza wakati wa hafla hiyo na kutoa ahadi kwa kilia Timu
ikishinda mchezo wao huo wa awali itazawadiwa shilingin Milioni Tano kwa
ushindi wowote ule,wakati wa hafla ya kukabidhi fedha za tiketi za
mchezo huo Kampuni yake imenunua tiketi zote zenye thamani ya shilingi
miliono tano kila moja na kutowa fursa kwa Wapenzi wa mchezo wa mpira
Zanzibar kuona mapambano hayo bure bila ya kiingilio.
Wachezaji wa Timu za JKU na Mafunzo wakiwa katika hafla hiyo katika ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Ocean View Kilimani Zanzibar.
Wachezaji wa Timu za JKU na Mafunzo wakiwa katika hafla hiyo katika ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Ocean View Kilimani Zanzibar.
Mshauri wa Kisheria wa Makampuni ya
Hoteli ya Zanzibar Ocean View Zanzibar Mhe Abdalla Juma akizungumza
wakati wa hafla hiyo kwa niaba ya Kampuni hiyo kuhusiana na udhamini wa
mchezo huo kwa timu za JKU na Mafunzo. na kutowa Salamu za Mkurugenzi
Mkuu wa Makampuni hayo Amani Ibrahim Makungu.
Meneja wa Makampuni ya Hoteli ya
Zanzibar Ocean View Zanzibar Jacob Makundi akimkabidhiwa Tiketi ya
Mchezo wa JKU na Gaborone United Club na Kiongozi wa Timu ya JKU Khamis
Mohammed, mchezo utakaofanyika katika Uwanja wa Amaan Zanzibar, Kampuni
ya Zanzibar Ocean View Imenunua tiketi hizo zote za mchezo huo na kutowa
fursa kwa Wananchi na Wapenzi wa Michezo Zanzibar kujionea Michuano
hiyo ya CAF kujionea bure. makabidhiano hayo yamefanyika katika Ukumbi
wa hoteli hiyo Kilimani Zanzibar
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269