Breaking News

Your Ad Spot

Feb 8, 2016

MAHAKAMA YAPOKEA SH. BILIONI 12.3 ZILIZOAHIDIWA NA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT.JOHN POMBE MAGUFULI.

mah1
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango (katikati) akimkabidhi Mtendaji Mkuu wa Mahakama Hussein Katanga (kushoto) mfano wa hundi wakati wa makabidhiano ya fedha hizo mbele ya waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju.
mah2
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango (katikati) akimkabidhi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju (kulia) mfano wa hundi wakati wa makabidhiano ya fedha hizo mbele ya waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama Hussein Katanga.
mah3
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango (katikati) akiongea na waandishi wa habari wakati wa makabidhiano ya fedha zilizotolewa kwa Mahakama leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju na kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango (kushoto).
mah4
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju (kulia) akitoa shukrani baada ya kupokea mfano wa hundi aliyopokea kwa lengo la kusaidia mahakama leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango.
mah5
Mtendaji Mkuu wa Mahakama Hussein Katanga akitoa shukrani baada ya kupokea mfano wa hundi aliyopokea kwa lengo la kusaidia mahakama leo jijini Dar es salaam. Katikati ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile na kulia ni  Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango.
mah6
Baadhi ya waandishi wa habari wakiendelea na kazi yao wakati wa makabidhiano ya fedha hizo mbele ya waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.
Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO
………………………………………………………………………………………………………..
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO.
 Dar es salaam.
Serikali imeikabidhi Mahakama ya Tanzania kiasi cha Sh.bilioni 12.3 zilizoahidiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Sheria kwa lengo la kuiwezesha Mahakama kuimarisha utendaji kazi na kutekeleza majukumu yake inapasavyo.
Akikabidhi fedha hizo mbele ya waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango amesema kuwa fedha zilizokabidhiwa kwa Mahakama ni mwitikio wa kutekeleza ahadi ya Rais aliyoitoa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria Duniani Januari 4, 2016.
“Ni matumaini ya Serikali fedha hizo zitatumika vizuri na zitatumika kwa madhumuni yaliyokusudiwa” alisema Dkt. Mpango.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju amemshukuru Mhe. Rais kwa kwa kutekeleza ahadi aliyoitoa ndani ya siku nne na kuudhihirishia umma kuwa kauli mbiu ya “Hapa Kazi Tu” anaisimamia kwa vitendo.
Naye Mtendaji Mkuu wa Mhakama Hussein Katanga amesema kuwa fedha walizokabidhiwa  zitasaidia ujenzi wa mahakama nchini na zipo ndani ya bajeti ya mwaka 2015/2016 na watazitumia kulingana na malengo yaliyokusudiwa.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages