Breaking News

Your Ad Spot

Feb 7, 2016

KANALI DK,KIIZA BESIGYE: SWAHIBA WA MUSEVENI ALIYEGEUKA ADUI KWA KUUTAKA URAIS WA UGANDA

Historia ya Besigye
Kizza Besigye Warren Kifefe alizaliwa Aprili 22, 1956, eneo la Rukungiri, Uganda. Ni kanali wa zamani wa Jeshi la Uganda, mwenyekiti wa Forum for Democratic Change (FDC), na amegombea katika uchaguzi wa rais nchini Uganda mwaka 2001, 2006 na mwaka huu 2011.
Maisha ya awali na kazi
Besigye, mtoto wa pili katika familia ya watoto sita, alisoma shule ya msingi Kinyasano na Mbarara Junior. Wakati akiwa shule ya msingi, wazazi wake wote walifariki. Alimaliza elimu ya sekondari katika shule ya Kitante na baadaye sekondari ya juu katika shule ya Kigezi.
Mwaka 1975 alijiunga na Shule ya Tiba ya Chuo Kikuu cha Makerere na kufuzu shahada ya udaktari mwaka 1980.
Baada ya kufanya kazi ya kutibu katika Hospitali ya Aga Khan ya Nairobi, aliacha na kuchukua mafunzo ya kijeshi kwa kujiunga na National Resistance Army kati ya mwaka 1980-1986 kwenye vita vya msituni dhidi ya serikali ya Milton Obote. Alikuwa akiwajibika kuangalia afya za wapiganaji na hasa Mwenyekiti, Yoweri Museveni.
Yoweri Museveni alipokuwa Rais mwaka 1986, Besigye, wakati huo akiwa na umri wa miaka 29, aliteuliwa Waziri wa Mambo ya Ndani. Mwaka 1988, aliteuliwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, na Kamisaa wa Siasa za Taifa.
Mwaka 1991, alikuwa Kamanda wa Kikosi cha kisasa wa Masaka, na mwaka 1993 akawa Mkuu wa ugavi na Uhandisi. Kabla ya kustaafu kutoka jeshi muda mfupi kabla ya uchaguzi wa 2001, Besigye alikuwa amefikia cheo cha Kanali na alikuwa Mshauri Mwandamizi wa Jeshi na Wizara ya Ulinzi.(VICTOR)
Mwaka 1998, Besigye alimuoa Winnie Byanyima, aliyekuwa Mbunge wa Manispaa ya Mbarara na mwanamke wa kwanza kuwa mhandishi mwanaanga nchini Uganda. Anselm Besigye, kijana wa kiume alizaliwa na Kizza Besigye na Winnie Byanyima, Septemba 1999.
Uchaguzi 2001
Kabla ya uchaguzi wa rais mwaka 2001, Besigye alijitokeza kuwa mpinzani wa sera za NRM ya Museveni na mfumo wa serikali wa “hakuna chama”, akiamini kuwa uongozi ulikuwa “haurekebishiki”, na kwamba “alitakiwa mtu kuchukua hatua na kuweka mambo sawa”. Alitaka kutazamwa upya kwa mfumo wa vuguvugu, na kubaki na utaratibu wa mpito, badala ya kuuhalalisha kama mfumo mbadala wa siasa.
Uchaguzi wa mwaka huo, Besigye, alionekana ndiye mpinzani pekee wa Museveni, alikuwa mmoja wa wagombea sita, wakati wa kampeni zilizokuwa na unyanyasaji mkubwa. Museveni alishinda uchaguzi wa urais, na matukio ya vurugu yalitokea baada ya kutangazwa kwa matokeo.
Kurudi toka uhamishoni na kukamatwa
Oktoba 26, 2005, Besigye alirejea Uganda kutoka Afrika Kusini, alikokuwa akiishi baada ya kuondoka Uganda. Maelfu ya wafuasi wake walijipanga mitaani kutoka Uwanja wa Ndege wa Entebbe hadi mji mkuu, Kampala.
Alikamatwa Novemba 14, 2005, akituhumiwa kwa uhaini na ubakaji. Kesi ya uhaini ilimhusisha na madai yake ya kuhusishwa na waasi wa vikundi vya LRA na PRA, na mashtaka ya ubakaji ilihusishwa na madai ya tukio la Novemba 1997 kati yake na binti wa rafiki yake.
Kukamatwa kwake kulifuatia maandamano na vurugu jijini Kampala na miji nchini kote. Waandamanaji waliamini kuwa mashtaka yaliundwa kumzuia Besigye kugombea rais katika uchaguzi wa 2006.
Februari uchaguzi 2006
Uchaguzi mkuu wa 2006 ulishuhudia chama cha FDC kama chama kikuu cha upinzani na Besigye kama mpinzani kuu dhidi ya Museveni kwenye urais. Museveni alichaguliwa kwa kipindi kingine cha miaka mitano, kwa asilimia 59 dhidi ya asilimia 37 za Besigye. Besigye, aliyakataa matokeo kwa madai ya kuwepo udanganyifu.
Mahakama Kuu ya Uganda ilitoa maamuzi kuwa uchaguzi huo ulikuwa umefunikwa na vitisho, vurugu, kuwagawa wapigakura, na makosa mengine. Hata hivyo, Mahakama ilimpitisha Museveni kwa kura 4-3 kuzingatia matokeo ya uchaguzi.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages