Mwanamke akiokolewa.
WATU
wawili wameokolewa wakiwa hai kutoka kwenye vifusi vya jengo
lililoporomoka kufuatia tetemeko la ardhi mjini Tainan, Taiwan.Wa kwanza
alikuwa mwanamke ambaye maafisa wanasema alipatikana chini ya mwili wa
mumewe. Mwili wa mtoto wao wa umri wa miaka miwili ulipatikana karibu
nao.
Mwanaume baada ya kuokolewa.
Muda
mfupi baadaye, mwanamume pia alipatikana akiwa hai, vyombo vya habari
nchini humo vimeripoti.Watu 37 walifariki baada ya tetemeko la ardhi la
kipimo cha Richter 6.4, kukumba taifa hilo.Wengi wa waliofariki walikuwa
katika jumba la Weiguan Jinlong, ambapo zaidi ya watu 100 bado
wanaaminika kukwama kwenye vifusi.
Ghorofa liliporomoka
Mwanamke
aliyeokolewa, Tsao Wei-ling, aliokolewa Jumatatu asubuhi, mbunge wa
eneo hilo Wang Ting-yu alinukuliwa akisema na shirika la habari la
Reuters.Alikuwa bado hajapoteza fahamu na alikimbizwa
hospitalini.Waokoaji wanasema ni kana kwamba mwili wa mumewe ulimkinga
dhidi ya nguzo iliyowaangukia.Watu 310 wameokolewa kufikia sasaJamaa
watano wa familia hiyo bado hawajulikani waliko.Mwanamume huyo mwingine
aliyeokolewa alikuwa akizungumza na waokoaji usiku wote kabla ya
kuokolewa mchana.
Msichana wa umri wa miezi sita aliyeokolewa akiwa hai awali alifariki baadaye akitibiwa hospitalini.
Jumba
la Weiguan Jinlong (Dragoni wa Dhahabu) lilikuwa na ghorofa 17.
Uchunguzi unafanywa kubaini iwapo udhaifu katika ujenzi wake ulichangia
kubomoka kwake.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269