Ile
vita ya wasanii kugombania majina ya wanyama imezidi kumake headline
kila kukicha na kuzua gumzo kwenye mitandao ya kijamii huku wakiwaacha
mashabiki na maswali kichwani ya nani mmiliki halali wa majina hayo?
Vita hiyo ya majina ya wanyama ilianzia
kwa msanii Mr Blue akimtuhumu Diamond kutumia jina la Simba japo
hakumtaja wazi wazi ila post yake ilijieleza, hivi karibuni imeibuka
vita nyingine kati ya msanii Dudubaya ambaye anamtuhumu msanii Shetta
kutumia jina lake la Mamba na kumtaka aache mara moja kabla hajamfanyia
kitu kibaya,
Mtembezi.com inakuletea sababu ambazo msanii Dudubaya amezitoa kupinga msanii Shetta kutumia jina lake la Mamba kama ifuatavyo.1.Hili
jina ni lake pekee na ukimya wake kwenye Game siyo sababu ya mtu
kuchukua jina lake na ametoa mfano kuwa wasanii kama Jarule na
DMX hawasikiki tena lakini haiwezekani mtu kuja kujiita Jarule au DMX.
2.Jina hilo la Mamba huwa analitumi
kibiashara pale akifungua biashara yake yeyote mfano Bar, Saloon n.k
huwa anatumia jina hilo kwahiyo tayari ni brand yake ambayo mwingine
hafai kuitumia.
3.Muonekano wa Shetta haufanani kabisa na jina hill na kamwe hawezi kuwa mamba,labda ajiite Kenge.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269