Makamu
Mkuu wa Chuo cha African Graduate University, Askofu Profesa Stephano
Nzowa (kulia), akizungumza katika mahafali ya pili ya chuo hicho
yaliyofanyika Dar es Salaam juzi.Kushoto ni Mkuu wa chuo hicho, Profesa
Timothy Kazembe kutoka nchini Zambia na mgeni rasmi wa mahafali hayo,
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani Tanzania (FCC), Dk. Fredrick Ringo.
Mkurugenzi
Mkuu wa Tume ya Ushindani Tanzania (FCC), Dk. Fredrick Ringo, ambaye
alikuwa mgeni rasmi akihutubia katika mahafali hayo.
Wahitimu wa chuo hicho wakiwa wamejipanga tayari kwa kuingia ndani kuanza kwa shughuli mbalimbali za mahafali hayo.
Ndugu na jamaa na wageni waalikwa kwenye mahafali hayo.
Wahitimu hao wakishiriki kuimba wimbo wa taifa.
Mahafali yakiendelea.
Taswira katika ukumbi wa mahafali.
Waliotoa huduma katika mahafali hayo wakiwa katika pozi.
Waimbaji wa nyimbo za injili wakitoa burudani.
Makamu
Mkuu wa Chuo hicho, Askofu Profesa Stephano Nzowa akimvika kofia
Mwimbaji wa nyimbo za injili, Stella Joel wakati akimtunuku Tuzo ya
Heshima ya Shahada ya Uzamili ya Mahusiano katika mahafali hayo. Kushoto
ni Mkuu wa Chuo hicho kutoka nchini Zambia, Profesa Timothy Kazembe.
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani Tanzania (FCC), Dk. Fredrick Ringo akimpongeza mwimbaji Stella Joel kwa kupata tuzo hiyo.
Na Dotto Mwaibale
WAHITIMU
wa Chuo Kikuu cha African Graduate University katika ngazi mbalimbali
wametakiwa kutumia elimu waliyopata kwa ajili ya wananchi na taifa kwa
ujumla.
Mwito
huo ulitolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani Tanzania (FCC),
Dk. Fredrick Ringomgeni aliye kuwa mgeni rasmi katika mahafali ya pili
ya chuo hicho yaliyofanyika Dar es Salaam juzi.
"Nawaombeni
sana elimu mliyopata itumieni kwa ajili ya kuinua maisha ya familia
zetu, wananchi na taifa kwa ujumla na si vinginevyo" alisema Dk.Ringo.
Makamu
Mkuu wa chuo hicho Askofu Profesa Stephano Nzowa aliwata wahitimu hao
kuendelea kujiendeleza kielimu hadi kufikia ngazi mbalimbali za juu.
Nzowa
alisema watu wengi wamekuwa wakijiendeleza kielimu wakiwa na matumaini
ya kuja kupata kazi nzuri jambo ambalo alisema ni bahati.
"Msisome
kwa ajili ya kuja kupata kazi nzuri bali someni ili kujiongezea uelewa
wa mambo mengi ambayo yatawasaidieni kuanzisha miradi mbalimbali ya
kuwaingizia fedha" alisema Nzowa.
Profesa
Nzowa alisema chuo hicho chenye makao makuu yake nchini Sieralaoni kipo
katika nchi kadhaa barani Afrika na kwa Tanzania kinajengwa
Wanging'ombe mkoani Njombe na kuwa mahafali hayo ni ya 25 na kwa hapa
nchini ni ya pili.
Mkuu
wa chuo hicho Profesa Timothy Kazembe kutoka nchini Zambia alisema
lengo lao ni kufungua chuo hicho katika nchi mbalimbali duniani ili
wanafunzi kujua mambo mbalimbali yakiwemo ya kijamii na ya mungu.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269