Breaking News

Your Ad Spot

Feb 11, 2016

AMISOM YAFICHUA MBINU ZA AL SHABAB

Jeshi la Amisom katika mji wa Barawe,  5 october 2014.
Vikosi vya Umoja wa Afrika nchini Somalia, AMISOM, vimesema kuwa kundi la Al-shabab lenye uhusiano na mtandao wa kigaidi duniani wa AL-Qaeda, limepanga kutekeleza mashambulizi nchini humo wakitumia mavazi ya wanajeshi wa umoja huo.
Amisom imesema katika taarifa yake kwamba mavazi hayo ya kijeshi yaliibiwa na wapiganaji jao wa Al shabab kutoka katika kambi ya kijeshi iliochini ya Umoja wa Afrika.
Taarifa hiyo ya Amisom imeongeza kuwa kundi hilo limepoteza muelekeo baada ya kuzidiwa nguvu sasa wamepanga kutekeleza mashambulizi dhidi ya raia na vikosi hivyo.(VICTOR)
Msemaji wa kundi hilo Aden Rage amethibitisha wapigaji wake kuwa na mavazi ya wanajeshi wa Umoja wa Afrika na kwamba wamepanga kutekeleza mashambulizi mfululizo ya kujitowa muhanga dhidi ya wanajeshi wa Amisom na Raia.
Kundi la Al shabab lemye mafungamano na mtandajo wa kigaidi duniani wa Al Qaeda limezidisha mashambulizi ya kujitowa muhanga katika siku za hivi karibuni na limetishia kuendeleza mashambulizo hayo ya kujitowa muhanga.
Amisom inasema ipo tayari kukabiliana na vitisho vya Al Shabab, kundi ambalo kwa sasa limepoteza nguvu kubwa baada ya kusambaratishwa katika miji kadhaa iliokuwa ikikalia.CHANZO:RFI

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages