UKITAJA
wakongwe na wakali wa sauti barani Afrika usipomtaja mwanamuziki wa
dansi kutoka Kongo, Jules Shungu Wembadio Pene Kikumba ‘Papa Wemba’,
utakuwa umekosea sana!
Wemba ni
mkongwe katika sanaa na muziki lakini sauti yake tamu na nzuri bado iko
vilevile licha ya umri kuonekana umemtupa mkono.
HISTORIA YAKE
Alizaliwa mwaka 1949 katika eneo la Lubefu mkoani Sankuru katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
MUZIKI WAKE UNA MAJINA KIBAO
Ni
mwanamuziki wa miondoko ya Lese- Rhumba ambayo baadaye ilijulikana kama
Soukous, Afro Pop Soukous, African Traditions na Central African.
NYIMBO ALIZOIMBA
Zipo
nyimbo na albamu nyingi alizofanya miongoni mwao ni pamoja na Pauline
alioufanya mwaka 1970 akiwa na Kundi la Zaiko Langa Langa mwaka 1995
aliachia albamu ya Emotion ikiwa na wimbo mkali wa Show Me The Way,
mwaka 1996 alifanya Wimbo wa Wake-Up 1996 akishirikiana na Koffi
Olomide, mwaka 2014 aliachia albamu ya Maître D’école-Teacher.
Nyingine ni Esclave, Maria Valencia, Lingo Lingo, Madilamba na Mwasi.
UMAARUFU WAKE
Wemba ni
mwanamuziki maarufu sana barani afrika na hata duniani. Anatajwa kama
mmoja wa wasanii wa kwanza walioanzisha Bendi ya Soukous Zaiko Langa
Langa mwaka 1969 mjini Kinshasa akiwa na wanamuziki kama Nyoka Longo
Jossart, Manuaku, Pepe Felly, Evoloko na wengineo.
Mwaka
1977 alianzisha Bendi ya Viva la Musica akiwa na vijana wenye vipaji
kutoka kijijini kwao na kufanikiwa kuachia nyimbo kama Mere Superieure,
Mabele Mokonzi, Bokulaka na zinginezo.
NI MUIGIZAJI
Mbali na
uimbaji, Wemba pia ni muigizaji na alishawahi kushiriki katika filamu ya
La Vie Est Belle- Maisha ni Bora iliyofanikiwa sana nchini Zaire (Kongo
kwa sasa) mwaka 1987.
SKENDO
Mwaka
2003 alishukiwa kuhusika katika mtandao ambao inadaiwa walivusha mamia
ya wahamiaji haramu kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (zamani
Zaire) hadi Ulaya, Papa Wemba alikamatwa nyumbani kwake mjini Paris na
kufungwa jela miezi mitatu na nusu na baadaye kuachiwa baada ya
kutokupatikana na hatia, ndani ya mwaka huo aliachia albamu ya Somo Trop
ikiwa na wimbo unaozungumzia kile kilichomkuta maishani mwake.
HIVI KARIBUNI
Mkali
huyo wa sauti, hivi karibuni alitua Bongo kwenye Tamasha la KARIBU MUSIC
FESTIVALS 2015 lililofanyika Novemba 6, Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani
na kuacha historia ya aina yake kutokana na kutozeeka sauti na kuonesha
umahiri wa hali ya juu katika uimbaji.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269