Meneja
Mawasiliano wa Kampuni ya Tigo, John Wanyancha akiongea na waandishi
wa habari (hawapo pichani), katika hafla ya kuzindua msimu mpya wa mbio
za Kilimanjaro Marathon 2016. Tigo wametoa zaidi ya shilingi milioni 200
kwa ajili ya mbio hizo.
Mkurugenzi
Msaidizi wa Michezo Wizara ya Habari Vijana, Utamaduni na Michezo, Alex
Nkenyenge (wa tatu kulia), pamoja na wadhamini wa Kilimanjaro Marathon
2016, wakifyatua fataki za karatasi ikiwa ni ishara ya kuzindua
maandalizi ya mbio hizo Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi wa
mashindano hayo, John Bayo
Mkurugenzi wa mashindano hayo, John Bayo (kulia), akizungumza katika uzinduzi huo.
Wadau wa michezo na waandishi wa habari wakiwa kwenye mkutano huo.
Mkurugenzi
Msaidizi wa Michezo Wizara ya Habari Vijana, Utamaduni na Michezo, Alex
Nkenyenge (katikati), akizungumza na wadau wa michezo wakati akizindua
maandalizi hayo ya Kilimanjaro Marathon 2016.
Wanahabari wakichukua taarifa za uzinduzi huo.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269