Breaking News

Your Ad Spot

Nov 12, 2015

IDADI YA WAKIMBIZI WA MALI WALIOKO NIGER YAONGEZEKA



4563097de6e277b8971291dd504eea7d_L

Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) limetangaza kuwa idadi ya wakimbizi raia wa Mali wanaokimbilia nchini Niger imeongezeka kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa.
Msemaji wa UNHCR, Leo Dobbs amesema, katika kipindi cha kati ya mwezi Oktoba hadi mwanzoni mwa mwezi huu wa Novemba idadi ya wakimbizi kutoka Mali waliokimbilia nchini Niger imeongezeka na kufikia 4,000, kiwango ambacho ni cha juu zaidi tangu yalipozuka mapigano nchini Mali mwaka 2012 hadi sasa.
Dobbs ameongeza kuwa kwa sasa idadi ya wakimbizi hao imefikia watu 54,000 na kuna wakimbizi wengine 3,000 wanaotarajiwa kuongezeka.
Msemaji wa UNHCR amefafanua kuwa licha ya serikali ya Mali na wapinzani wanaobeba silaha kusaini makubaliano ya amani mwezi Juni mwaka huu baada ya duru kadhaa za mazungumzo chini ya upatanishi wa Algeria lakini kumekuwepo na matukio kadhaa ya ukiukaji makubaliano hayo na mapigano ambayo yamekuwa yakishuhudiwa katika maeneo ya kaskazini mwa Mali.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages