Aliyekuwa
Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk. Tulia Ackson Mwansasu hivi
punde amechaguliwa kuwa Naibu Spika wa Bunge la 11 la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania baada ya kupata jumla ya kura 250 sawa na 71.2%
huku mpinzani wake Magdalena Sakaya (CUF) akipata kura 101 sawa na
28.8%.
Dk. Tulia
hivi karibuni aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dk. John Pombe Magufuli kuwa mbunge baada ya kutenguliwa uteuzi wake
kama Naibu Mwanasheria Mkuu.
Kabla ya
uteuzi huo, Dk. Tulia alikuwa akiwania nafasi ya Uspika wa bunge baada
ya kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) lakini yeye na mgombea
mwenzake Abdullah Ali Mwinyi walijitoa na kumuachia Job Ndugai awanie
nafasi hiyo.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269