Breaking News

Your Ad Spot

Oct 4, 2015

MAGUFULI NOMAA!! ATIKISA SINGIDA,SHUHUDIA HAPA BALAA LAKE,PUSH UP KAMA KAWAIDA

Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwasili kwenye viwanja vya mikutano vya Peoples kuhutubia wakazi wa Singida mjini.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi Singida mjini kwenye uwanja wa mikutano wa Peoples ambapo aliwaambia wakazi hao kuwa ataibadilisha Singida na kuufanya kuwa mji wa Biashara, pia aliwaambia vijana wanafunzi wa vyuo kuwa atahakikisha wanapata mikopo kwa wakati, mikopo kwa vijana na wakina mama .

Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia maelfu ya wakazi wa Singida mjini waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa kampeni za CCM.
Mgombea wa Urais kwa kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akitoa salaam za shukrani kwa Mbunge wa Singida mjini anayemaliza muda wake Ndugu Mohamed Dewji (kushoto) na Mkuu wa mkoa wa Singida Dokta Parseko Vicent Kone kwenye mkutano wa kampeni za CCM.

Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akimkabidhi mgombea wa ubunge wa jimbo la Singida kitabu cha Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya Peoples.


Mbunge wa Viti Maalum mtarajiwa Aysha-Rose Matembe akiwasalimu wakazi wa Singida mjini waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni za CCM.


Kutoka kulia ni Mgombea Ubunge wa Jimbo la Iramba Mwigulu Nchemba akipiga push ups pamoja na mgombea ubunge wa jimbo la Singida mjini Ndugu Mussa Sima (katikati) na Mgombea wa Ubunge wa Jimbo la Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu.


Wakazi wa Singida mjini wakifuatilia mkutano wa kampeni wa Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli.


Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Singida Diana Chilolo akihutubia wakazi wa Singida mjini waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni za kumnadi Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli.


Mgombea Ubunge wa jimbo la Iramba Mwigulu Nchemba akihutubia wakazi wa Singida mjini waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli.


Mgombea ubunge wa jimbo la Bumbuli Ndugu January Makamba akihutubia wakazi wa Singida mjini waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa kampeni za Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli.


Mgombea Ubunge wa Jimbo la Singida Kaskazini Ndugu Lazaro Nyalandu akihutubia wakazi wa Singida mjini kwenye mkutano wa kampeni za kumnadi Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli.


Mbunge wa Jimbo la Singida mjini anayemaliza muda wake Ndugu Mohamed Dewji akihutubia wakazi wa Singida mjini kwenye mkutano wa kampeni za Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli. 


Umati wa wakazi wa Singida mjini waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni za Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli


Msafara wa Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli ukiwasili kata ya Sepuka .


Mwigulu Nchemba akimkaribisha Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli alipowasili Sepuka.


Wakazi wa Sepuka wakishangilia ujio wa Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli.


Mgombea Ubunge wa Jimbo la Iramba Mhe. Mwigulu Nchemba akizungumza na Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli kabla ya kuhutubia wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye viwanja vya shule ya msingi Kiomboi Bomani.


Mgombea Ubunge wa Jimbo la Iramba Mhe. Mwigulu Nchemba akihutubia kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Kiomboi Bomani.


Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa shule ya msingi Kiomboi Bomani.


Wakazi wa Kiomboi wakimsikiliza Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli.


Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiondoka eneo la Mto Ndulumo baada ya kukagua daraja ambalo kwa sasa halitumiki baada ya kuathirika na mafuriko ambapo aliwaahidi wananchi wa kijiji cha Msingi Kidi kuwa daraja hilo litatengenezwa mapema.


Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akimnadi mgombea ubunge wa jimbo la Iramba Mashariki Ndugu Allan Joseph Kiula kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Nduguti.


Wakazi wa Singa wakimsikiliza Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli

Picha kwa hisani ya Kamerayangu blog

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages