Rais Kikwete akutana Alpha Konare Mjumbe wa AU Sudan ya Kusini
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete
akimkaribisha na kufanya mazungumzo na Mhe.Alpha Oumar Konare ambaye ni
msuluhishi wa Umoja wa Afrika(AU) katika mgogoro wa Sudan ya Kusini
ikulu jijini Dar es Salaam jana.Mbali na majadiliano yaliyohusu vita vya
wenyewe kwa wenyewe katika taifa changa la Sudan ya Kusini Bwana Konare
ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Mali(1992-2002) na mwenyekiti mstaafu wa
Kamisheni ya Umoja wa Afrika alimweleza Rais Kikwete umuhimu wa kutumia
Kiswahili katika mikutano ya Umoja wa Afrika.(picha na Freddy Maro)
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269