Breaking News

Your Ad Spot

Aug 19, 2015

NAPE NA MTANDA WACHUKUA FOMU ZA TUME YA UCHAGUZI KUWANIA UBUNGE MKOANI LINDI


  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akisalimina na wananchi waliojitokeza kumsindikiza kwenda kuchukua fomu za uteuzi wa ubunge za Tume ya Taifa ya Uchaguzi Nape Nnauye ndie  mgombea aliyependekezwa na Chama Cha Mapinduzi kugombea jimbo la Mtama mkoani Lindi.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimiana na Katibu Mwenezi wa kata ya Namangare Mzee Evod  nje ya ofisi za CCM mkoa Lindi,muda mfupi kabla ya kwenda kuchukua fomu za uteuzi wa ubunge za Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akizungumza na kamati ya siasa ya mkoa pamoja na wagombea ubunge wa CCM kutoka majimbo yote ya mkoa wa Lindi kabla ya kumsindikiza kwenda kuchukua fomu za uteuzi wa ubunge za Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akitoka kwenye ofisi za CCM mkoa wa Lindi akiongozana na Said Mtanda kuelekea kwenye Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Lindi kuchukua fomu za uteuzi wa ubunge za Tume ya Taifa ya Uchaguzi
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye ambaye ndiye mgombea wa CCM jimbo la Mtama pamoja na Said Mtanda anayegombea kwa jimbo la Mchinga wakiwasili kwenye ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Lindi kuchukua fomu za uteuzi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akikabidhiwa fomu za uteuzi kwa nafasi ya ubunge na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Olliver Vavunge.
Mbunge wa Jimbo la Mchinga Said Mtanda akipokea fomu za uteuzi kwa nafasi ya ubunge na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Olliver Vavunge.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages