Breaking News

Your Ad Spot

Aug 2, 2015

MAKONGORO MAHANGA AMFUATA LOWASSA BAADA YA KUSHINDWA KURA ZA MAONI UBUNGE CCM

theNkoromo Blog, Segerea
Aliyekuwa Mbunge wa Segerea, aliyekuwa pia Naibu Waziri wa Kazi na Maendeleo ya Vijana,  Dk. Milton Makongoro Mahanga, ameamua kumfuata Chadema, Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa.



Mahanga, ametangaza kuhamia Chadema, leo, baada ya kushindwa katika kura za maoni za CCM,  wakati akijaribu kutetea ubunge wake katika jimbo hilo, na kusema atahamia Chadema aliko Lowassa, ikiwa chama hicho kitamkaribisha.

Hatua hiyo imehitimisha, tetesi za siku nyingi zilizokuwa zikidai kuwa Mahanga amekuwa mfuasi wa Lowassa kwa mda mrefu, katika siasa za Tanzania.

Lowassa pia alitangaza kuhamia Chadema wiki iliyopita, baada ya jina lake kukatwa mjini Dodoma, katika kinyang'anyiro cha kuwania kuteuliwa kugombea Urais kwa tiketi ya CCM katika uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu. Pichani, Mahanga akizungumza na waandishi wa habari kutangaz uamuzi wake wa kwenda Chadema.


No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages