Makamu Mkuu wa Chuo kikuu cha Dar
es Salaam Profesa Rwekaza Mukandala akimkabidhi Rais Dkt . Kikwete cheti cha Shahada ya Heshima ya Doctor of Laws (Honoris Causa)
wakati wa hafla fupi ya kumkabidhi Rais joho na cheti iliyofanyika ikulu
jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na maprofesa waandamizi wa chuo
hicho.Tayari Rais Kikwete alishatunukiwa shahada hiyo katika mahafali ya
41 ya UDSM yaliyofanyika Octoba mwaka 2011.
Profesa Agnes Mwakaje wa Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam akimvika kofia ya kitaaluma Rais Dkt. Kikwete wakati wa hafla fupi ya kumkabidhi Rasmi Rais Joho na
cheti cha shahada ya heshima ya Doctor of Laws (Honoris Causa) ikulu
jijini Dar es Salaam.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar
es Salaam Profesa Rwekaza Mukandala akisoma maelezo mafupi baada yeye
na jopo la maprofesa waandamizi wa chuo hicho kumkabidhi Joho la taaluma
na cheti cha Shahada ya heshima ya Doctor of Laws (Honoris Causa) ya chu
kikuu cha Dar es Salaam wakati wa hafla iliyofanyika ikulu jijini Dar
es Salaam
Rais Dkt.
Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha
Dar es Salaam Profesa Rwekaza Mukandakla pamoja na maprofesa waandamizi
wa chuo hicho muda mfupi baada hafla fupi ya kumkabidhi Rais Joho na
Cheti cha Shahada ya Heshima ya Doctor of Laws (Honoris Causa)
ikliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam leo (picha na Freddy Maro)
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269