Mjumbe
Mkutano Mkuu wa CCM Manispaa ya Singida, Hasan Mazala akionesha vijana
fomu yake ya kuwania ubunge Jimbo la Singida Mjini jana kwenye ukumbi wa
mikutano wa CCM Mkoani Singida.
Mazala akiwaasa vijana kufanya kazi kwa nguvu katika jimbo hilo.
Mkinipa nafasi ya kuwatumikia mambo yatanyooka namna hii.
Mgombea
wa nafasi ya Ubunge Jimbo la Singida Mjini Hassan Philipo Mazala
akisistiza jambo kwa vijana waliomsindikiza kuchukua fomu.
Baadhi
ya vijana wakiwa katika picha ya pamoja na Hassan Mazala nje ya jengo
la makao makuu ya CCM Mkoa wa singida mara baada ya kuchukua fomu.(PICHA
ZOTE NA HILLARY SHOO).
Na Hillary Shoo, SINGIDA
MJUMBE
wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa (MNEC) Manispaa ya Singida,Hassan Mazala
amechukua fomu ya kuwania Ubunge Jimbo la Singida Mjini ..
Akizungumza
na kundi la Vijana wa CCM kwenye ukumbi mdogo jana, Mazala amesema kuwa
amefungua ukurasa mpya wa maisha yake kwa kuwania nafasi hiyo
iliyoachwa wazi na Mohammed Dewji aliyestaafu.
‘Nimejipima
nikaona ninaweza kuvaa viatu vilivyoachwa wazi na Dewji kwani katika
kipindi chote alichukuwa Mbunge nilishirikiana nae katika kuyatekeleza
yale yote aliyonituma kama msaidizi wake wa karibu.” Alisema Mazala.
“Nimekuwa
Kiongozi kwa muda mrefu katika ngazi mbalimbali kuanzia kwenye vijiji
,Kata, Wilaya, Mkoa na sasa Taifa, hivyo nina uwezo wa kutosha na
nimekomaa kisiasa katika kufanya kazi hii ya Ubunge bila wasiwasi
wowote pale alipoachia Dewji” Alisisitiza.
Aidha
alisema anazifahamu changamoto zinazolikabili Jimbo hilo kwani
ametembea kona zote na kujionea hali halisi ya wananchi
wanavyojishigulisha na shughuli za kijamii.
“Nina
Moyo wa dhati kabisa wa kuwatumikia, ninaombeni mnibebe, najua
yamesemwa mengi sana juu yangu katika kipindi ambachio nimlikuwa nafanya
kazi na MO, lakini yapuuzeni hayo kwani hayana ukuweli wowote ni chuki
binafsi tu.” Alisema huku akishangiliwa na kundi la vijana linalojiita
team Mazala.
Hata
hivyo Mazala ambaye ana uwezo mkubwa wa kutawa jukwaa alisema kamwe
hatawaanguisha wananchi wa Jimbo hilo huku akitumia misamiati Zimwi
likujualo, Usiache mbachao na mwokoto kuni porini huota moto pamoja.
Akitangaza
kutogombea tena Ubunge mapema Julai 08 mwaka huu mjini Singida Dewji
alimsifu Mazala kwa kusema kuwa ni mchapa kazi, mwaminifu, mwadilifu na
ana moyo wa kujitolea kwani aliweza kusimamia kazi zake zote bila ya
matatizo yoyote.
“Na
pia ninapenda kumshukuru kipekee mtu mmoja ambaye bila yeye mafanikio
yangu ya kiuongozi niyoyopata hapa Singida yasingeweza kufanikiwa vizuri
bila ya yeye.” Alisema Dewji katika taarifa yake hivi karibuni.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269