Breaking News

Your Ad Spot

Mar 4, 2015

KATIBU MKUU WIZARA YA HABARI, VIJANA , UTAMADUNI NA MICHEZO AHIMIZA WATUMISHI WAKE KUENDELEA KUWA WABUNIFU KATIKA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga akizungumza na watumishi wa Wizara hiyo (hawapo pichani) wakati wa kikao kazi cha kawaida ambacho ufanyika kila baada ya miezi mitatuKikao hicho kimefanyika jana katika ukumbi wa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Elisante Ole Gabriel na kulia ni Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Magreth Mtaki. 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga akisisitiza jambo kwa  watumishi wa Wizara hiyo (hawapo pichani) wakati wa kikao kazi cha kawaida kilichofanyika  jana katika ukumbi wa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Elisante Ole Gabriel. 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Elisante Ole Gabriel akafafanua jambo wakati wa kikao cha Watumishi wa Wizara hiyo kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam.Katikati  ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga na kulia ni Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Magreth Mtaki. 
Kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga, Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Wizara hiyo Bibi. Magreth Mtaki na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel wakifuatilia mada kuhusu bajeti ya Wizara iliyowasilishwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Sera na Mipango wa wizara hiyo Mwanzala Kayoka (hayupo pichani).
Mkurugenzi Msaidizi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Mwanzala Kayoka akiwasilisha mada kuhussu uelekeo wa Bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2014/15 na 2015/16 wakati wa kikao kazi cha kawaida baina ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo na watumishi wote kilichofanyika jana  katika ukumbi wa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. 
Mkuu wa Kitengo cha Sheria wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Ester Liwa akielezea jambo wakati wa kikao kazi cha kawaida baina ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo na watumishi wote kilichofanyika jana  katika ukumbi wa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. 
Ofisa Utamaduni kutoka Bodi ya Filamu Bib. Beatrice Sumari akielezea jambo wakati wa kikao kazi cha kawaida baina ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo na watumishi wote kilichofanyika jana  katika ukumbi wa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. 
Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakiwa katika kikao kazi kilichofanyika jana katika ukumbi wa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakiwa katika kikao kazi kilichofanyika jana katika ukumbi wa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. 

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages