Breaking News

Your Ad Spot

Jan 24, 2015

MUHONGO AJIUZULU, RAIS KIKWETE AFANYA MABADILIKO MADOGO BARAZA LA MAWAZIRI

NA BASHIR NKOROMO, DSM
WAKATI aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ametangaza kujiuzulu, Rais Jakaya Kikwete ametangaza marekebisho madogo ya Baraza lake la Mawaziri.

Taarifa iliyotangazwa na Katibu Mkuu Kiongozi  Ombeni Sefue leo, imesema, nafasi iliyoachwa na Profesa Muhongo sasa itashikwa na George Simbachewene, huku nafasi ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Oratibu na Bunge ikichukuliwa na Dk. Mary Nagu.

Kulingana na taarifa hiyo, aliyekuwa Waziri wa Chakula na Kilimo Christopher Chiza anakuwa Waziri wa Uwezeshaji na Uwezeshaji, huku Dk. Harisson Mwakyembe akipewa nafasi ya Uwaziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Waziri William Lukuvu anakuwa waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na Profesa Anna Tibaijuka kabla ya kujiuzulu kufuatia sakata la Tegeta ESCROW.

Naye Stephen Wasira katika mabadiliko hayo, anakuwa Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, wakati aliyekuwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta anakuwa Waziri wa Uchukuzi na Jenista Mhagama akipewa nafasi ya Uwaziri wa  Sera na Uratibu wa Bunge.

Taarifa imesema, aliyekuwa Waziri wa Sheria na Katiba Angela Kairuki anakuwa Naibu wa Ardhi Nyumba na Makazi,  huku Steven Masele akipata nafasi ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano.

Wengine ni Ane Kilango Malecela anayekuwa Naibu Waziri wa Elimu, Ummy Mwalimu Naibu Waziri wa Sheria na Katiba na Mwijage Naibu Waziri wa Nishati na Madini.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages