Breaking News

Your Ad Spot

Jan 22, 2015

HAKIELIMU: UTEKELEZAJI WA BRN KATIKA ELIMU BADO HAURIDHISHI

Na Fatuma Bashir
IKIWA ni mwaka mmoja sasa tango utekelezaji wa mpango wa matokeo  makubwa sasa BRN imeelezwa kuwa hali ya utekelezaji huo bado si ya  kuridhisha.


Imeelezwa kwamba baada ya ya mwaka 2013 Serikali ya Tanzania  kuzindua  mpango maalum  wa ufuatiliaji  utekelezaji  wa mipango na   na utoaji wa huduma  kwa umma unaojulikana kama BRN,  kwa lengo  la kusukuma  maendeleo na kuharakisha utekelezaji mipango  na kuleta  matokeo  yaliyokusudiwa  upesi  kama hatua ya mwanzo ya BRN,   ilichagua  sekta sita  za mfano ambazo ni  Kilimno. Maji,  Elimu, Nishati  na madini, Fedha na Usafirishaji.


Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Kaimu  Mkurugenzi wa Taasisi ya Haki Elimu, Bwana Godfrey Boniventura  alisema, licha ya serikali kuanza kufanya  na kutoa tathmini  ya  mpango huo kupitia jopo la  Kimataifa la Tathmini (IRP), Taasisi hiyo  kama mdau wa Elimu  imefanya tathmini  yake  ili kupima ufanisi  wa  matokeo ya mpango huo  katika sekta hiyo ya elimu kwa mwaka  mmoja  na kubaini kwamba matokeo bado si ya kuridhisha.


Alisema, katika  sekta ya elimu  yaliyopangwa kutekelezwa  katika  kipindi cha mwaka mmoja kati ya 2013/14,  ni pamoja na kuongeza   ufaulu hadi kufikia asilimia 70 mwaka 2014, kutoa ruzuku iliyopamgwa  kwa kila mwanafunzi, kutoa mafunzo ya uongozo kwa walimu 19035  kufikia Septemba 2013, mafunzo kwa walimu 12300 juu ya ufundishaji  wa KKK, kujenga nyumba 500 za walimu kwa shule za sekondari.
Mengine ni kukarabati miundombinu kwa shule 1200 za sekondari na  kuhakikisha kuwa uwiano wa mwanafunzi kwa kitabu unashuka kutoka  kitabu kimoja kwa wanafunzi watano hadi vutabu sita kwa mwanafunzi  mmoja.


Biniventura alisema japokuwa taarifa ya jumla ya jopo la IRP, inasema  mwelekeo wa utekelezaji wa BRN ni mzuri, katika ufuatiliaji uliofanywa  na Haki Elimu katika sekya ya elimu kwa karibu sana imebaini kuwa hali  ya utekelezaji wake bado si ya kuridhisha.


"Mathalani BRN ilipamnga kuongeza kiwango cha ufaulu kwa shule za  sekondari na msingi hadi kufikia asilimia 60 mwaka 2013 na silimia 70  mwaka 2014, pamoja na matokeo kuonyesha matokeo kuonyesha  ongezeko la ufaulu kutoka asilimia 50.6 (2012) hadi kufikia asilimia 50  (2013) kwa shule za sekondari na kutoka asilima 30.7 mwaka 2012  hadi asilimia 50.6 mwaka 2013 kwa shule za msingi, bado lengo la  asilimia 60 halikufikiwa", alisema  Biniventura na kuongeza kuwa,


"Hali hiyo inaonyesha kuwa lengo la ufaulu kwa shule za sekondari  kufikia asilimia 60 kwa mwaka 2013 limefanikiwa kwa asilimia karibu 79  na kwa asilimia 42 tu kwa shule za msingi".


Alisema hata hivyo ufaulu wa sekondari siyo wa kujivunia kwa sababu  matokeo ya mtihani wa mwaka 2013 yametumia viwango vipya vya  madaraja na hivyo haiwezekani kusema yametokana na utekelezaji wa  BRN.


Boniventura alisema kwa upande wa ruzuku BRN, imeshindwa kufikia  lengo la kupeleka ruzuku iliyokamilika katika mwaka wa fedha 2013/14  wakati shule za msingi zilipaswa kupokea wastani wa sh. 10,000 kwa  kila mwanafunzi lakini ni wastani wa sh. 3580 tu kwa kila mwanafunzi  uliofika shuleni na wastani wa sh. 16, 384 tu ukifika shule za sekondari  badala ya sh. 25,000 uliopangwa.


Alisema mwenendo huo wa utoaji ruzuku siyo dalili tu za kuyofikiwa  malengo ya BRn bali pia ni ishara hasi ya kufikia lengo la kuboresha  elimu hapa nchini kwa sababu ruzuku ya wanafunzi ndicho chanzo kikuu  cha mapato kwa shule za umma ambapo hutumika kununua vifaa vya  kufundishia na kujifunzia na kukidhoi gharama ndogondogo za  uendeshaji wa shule hivyo shule zimapokosa ruzuku zinashindwa  kunoresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia na hivyo kuathiri  ubora wa elimu itolewayo shuleni.


Boniventura alisema BRN pia ilikuwa imeazimia kuwa hadi kufikia  Septemba 2014 serikali itakuwa imefanya ukarabati na ujenzi wa  miundombinu kwa shule 792 lakini hadi kufikia Machi 2014 ni shule 56  tu ndizo zilikuwa zimefanyiwa ukarabati.


Alisema licha ya BRN kujikita katika ujenzi na ukarabati miundombinu  lakini changamoto ya ubovu wa miundombinu bado ni kubwa kwa shule  nyingi, takwimu za BEST, 2014 zinaonyesha kuwa wa shule za  sekondari kuna upungufu mkubwa wa maabara 1355 sawa na asilimia  94.8, za kilimo, maabara 4416 za baiolojia sawa na asilimia 76.4,  maabara za kemia 4461 sawa na asilimia 72.6 na maabara za Fiizikia  1024 sawa na asilimia 75.


Pia kuna upungufu wa nyumba 51187 za walimu sawa na asilimia 72,  madarasa 13591 sawa na asilimia 22.6 na matundu ya vyoo 44926  sawa na asilimia 40, hali ikiwa mbaya zaisi kwa shule za msingi ambapo  kuna upingufu wa vyoo 27,736 sawa na asilimia 60.3 ambapo uwiamo  wa wanafunzi wa tundu la choo ni 1:53 badala ya 1:23 kwa wavulana  na 1:51 kwa wasichana badala ya 1:20.


Alisema, pia kuna upunguzu wa madarasa 82,788 sawa na asilimia 41  ambapo uwiano wa wanafunzi kwa darasa ni 1:72 na tatizo ni kubwa  zaidi kwa mikoa ya Rukwa uwiano 1:84, Geita 1:126 na Mwanza 1:110,  upungufu wa nyumba za walimu 16,007 sawa na asilimia 79 na  madawati milioni 1.2 sawa na asilimia 37.7.


Boniventura alisema, serikali pia ilikusufdia kutoa mafunzo kwa walimu  19, 350 kwa shule za msingi na sekondari hadi ifikapo Septemba 2013  lakini taarifa za utekelezaji zinaonyesha kuwa hadi kufikia Aprili 2014  serikali iliweza kuwapatia mafumzo ya uomgozi walimu 3469 tu ambao  ni wa shule za sekondari na hivyo kuwa imetekeleza lengo hilo kwa  asilimia 18 tu.


Alisema changamoto kubwa inaonyesha kuwa walimu wa shule za  msingi ambao hadi kufikia Septemba 2014 hakuna hata mwalimu  aliyepatiwa mafunzo ya uongozi kati ya walimu 15,524 waliotarajiwa  kupatiwa mafunzo hayo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages