Breaking News

Your Ad Spot

Dec 16, 2014

VETA WAMETAKIWA KUHAKIKISHA WANAANDAA WANAFUNZI WA HOTELI NA UTALII WENYE VIWANGO VYA KIMATAIFA ILI KUKABILIANA NA USHINDA WA SOKO ULIOPO

Mkuu wa wilaya ya Arumeru Nyerembe Munasa akiwa anaongea wakati wa uzinduzi  wa baraza la ushauri wa chuo cha mafunzo ya hoteli na utalii cha mamlaka ya elimu ya mafunzo ya ufundi stadi (VHTTI) Kilichopo Njiro mkoani Arusha

baadhi ya watumishi wa VETA  akiwemo Mkurugenzi wa Veta, Mhandisi Zebadiah Moshi wakiwa wanabadilishana mawazo nje ya viwanja vya chuo  cha mafunzo ya hoteli na utalii


mkuu wa wilaya ya Arumeru akiwa anamkabidhi nyaraka ya kutendea kazi mmoja wa wajumbe wa baraza la chuo cha VHTTI ambaye ni mwakilishi wa chama cha wamiliki wa makampuni ya utalii(TATO) bw, Peter Lindstrone



wadau mbalimbali wakiwemo wajumbe wa chuo hicho wakiwa wanafatilia uzinduzi huo wa baraza la chuo kwa makini




mkurugenzi wa VETA wa kwanza  kulia Mkurugenzi wa Veta, Mhandisi Zebadiah Moshi akifuatiwa na mwenyekiti wa bodi  pamoja na mkuu wa wilaya ya Arumeru Nyerembe Munasa na wakwanza kushoto ni mkuu wa chuo cha VHTTI Flora Hakika wakibadilishana mawazo


waandishi wa habari mbalimbali wakiongea na mkuu wa wilaya mara baada ya uzinduzi huo wa baraza la ushauri wa  chuo cha  mafunzo  ya hoteli na utalii cha VHTTI

wageni waalikwa wakiwa wanafatilia uzinduzi huo kwa makini sana






Na woinde shizza ,Arusha

Baraza la ushauri la chuo cha  mafunzo ya hoteli na utalii (VHTTI) limetakiwa kuhakikisha linaandaa wanafunzi vyema na wenye viwango vya kimataifa   ili kukabiliana  na ushindani mkubwa ulioko katika sekta ya hoteli na utalii duniani.

Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Arumeru Nyerembe Munasa wakati akizindua baraza hilo  jana ndani ya chuo cha hoteli na utalii cha VHTTI kilichopo  nje kidogo ya jiji la Arusha .

Alisema kuwa kutokana na changamoto kubwa ya  hoteli zetu kuajiri watu kutoka nje ya nchi ikiwemo kenya na hata nchi za bara ya ulaya  kwa kile kinachodaiwa vijana wazawa kutokuwa na elimu ya kutosha  kuhusiana na sekta ya hoteli na utalii hivyo ni wajibu wao kuakikisha wanafundisha wanafunzi ili waweze kuwa na elimu ya kiwango cha kimataifa .

Alibainisha kuwa  wanatakiwa wahakikishe wanachuo ambao wanawafundisha wanakuwa na sifa zinazotakiwa huku akiongeza kuwa mafunzo wanayofundishwa yawe bora yanayokidhi maitaji ya ajira .

Aidha alisema kuwa iwapo watawafundisha wanafunzi hao vyema na kuwapa elimu inayoitajika kuoendana na soko hii itawasaida kupunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la ajira kwani wanafunzi hawa pindi watakapo maliza elimu yao itakuwa raisi kupata kazi kulingana na elimu walikuwa nayo.

''pia napenda kuwashauri  kuanzisha lunga zote za kimataifa katika chuo chenu ili mwanafunzi anaetoka katika chuo hichi aweze kuwasiliana na mgeni yeyote ambaye atakuja kutoka katika nchi yoyote huko kazini kwake anapoenda kwakweli inachekesha sana kuona mgeni anakuja alafu mwanafunzi anaanza kuongea lunga mfano ya kingereza kwa kukosea kosea au anaongea frechi kwa kukose  kosea''alisema  munasa

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Veta, Mhandisi Zebadiah Moshi  alisema kuwa    wao kama Veta wameamua kuanzisha chuo hichi cha  hoteli na utalii ili kuweza kupunguza tatizo la ajira ambalo linaendelea kwa vijana wengi.

Aliesema kuwa  chuo hichi  kitatoa mafunzo ya hoteli na utalii katika ngazi ya cheti na shahada  kwa wasimamizi na waangalizi wa hoteli zetu.

Naye mkuu wa chuo hicho   Flora Hakika alisema kuwa wataji taidi kuwafundisha wanafunzi  vyema na wataanza kwa kuaandaa mitaala mipya huku wakiwa wanaangalia zaidi  jinsi wenzetu wa nchi za nje wanavyo fanya pia watajitaidi  kulenga kupata maitaji ya soko linavyoitaji ili kuweza kuinua zaidi utendaji kazi  wa vijana wa kitanzania

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages