Breaking News

Your Ad Spot

Oct 20, 2014

MTUHUMIWA WA UGAIDI WA ULIPUAJI WA MABOMU ARUSHA AUAWA NA POLISI AKIJARIBU KUTOROKA

Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha,Liberatus Sabas
 Kiongozi wa  matukio ya ulipuaji wa mabomu na umwagiaji tindikali viongozi wa dini aliyejulikana kwa jina la Yahaya Hassani Omary ameuwawa na jeshi la polisi wakati alivyokuwa akijaribu kukimbia.



Akithitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoani Arusha  Liberatus Sabas  Alisema kuwa tukio hilo limetokea  October 19 majira ya saa tano na nusu  katika barabara ya babati mkoani Arusha wakati alipokuwa akijaribu kuwakimbia polisi.



Alisema kuwa mtuhumiwa huyo wa ugaidi alishikiliwa wiki mbili zilizopita  huko mkoani Morogoro  mara baada ya kutafutwa kwa muda mrefu na hapo jana alikuwa akipelekwa wilayani kondoa mkoani Dodoma  kwa ajili ya kwenda kuonyesha sehemu ambazo alikuwa ameficha mabomu mengine.

"mtuhumiwa huyu alikuwa anasakwa kwa muda mrefu bila mafanikio kwani alikuwa akai sehemu moja ila jeshi la polisi huko mkoani morogoro lilimkamata wiki mbili zilizopita na baada ya kufanyia mahojiano alisema ameficha mabomu mengine huko kondoa na jana alikuwakipelekwa kuonyesha ndipo alipotumia trikizake ambazo amefundishwa za ugaidi kwa kupiga gudo na kutaka kuwakimbia askari ndio akapigwa risasi mbili"alisema Sabas



Alitoa wito kwa wananchi kuendelea kuwafichua waovu  ili kuwaza kuteketeza matukio ya uhalifu
habari kwa hisani ya woindeshizza blog

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages