Breaking News

Your Ad Spot

Dec 22, 2011

MVUA NOMA DAR!

 Mkazi wa bonde la Jangwani Dar es Salaam, akihamisha vyombo baada ya eneo hilo kukumbwa na mafuriko jana, kufuatia mvua zilizonyesha tangu juzi.
  Mkazi wa Jwangwani akiogelea kwenye godoro kujiokoa baada eneo hilo kukumbwa na mafuriko.
 Barabara ya Morogoro, ikiwa imefunikwa na maji eneo la bonde la Jangwani Dar es Salaam, jana kufuatia mafuriko yaliyolikumba eneo hilo kutokana na mvua zilizoanza junyesha juzi.
 Nyumba na daladala vikiwa vimezingirwa na maji huku baadhi ya watu wakiwa juu ya paa za nyumba kujinusuru, baada ya eneo la bonde la Jangwani kukumbwa na mafuriko jana.
 Watu wakitembea kwa miguu baada ya magari walimokuwa wakisafiria kwenda Kariakoo na Posta kushindwa kuvuka eneo la daraja la jangwani kutokana na mafuriko jana.
 Eneo la Jangwani karibu na Ofisi za Kajima likiwa limefurika maji
 Barabara Bagamoyo ikiwa imemomonyoka karibu na daraja la Kawe, kutokana na mvua zilizonyesha jana. Hali hiyo imesababisha barabara kufungwa katika eneo hilo na hivyo magari kati ya Tegeta na
Mwenge ambayo hupita eneo hilo kulazimika kuishia hapo.
 Bajaji na pikipiki zisafirisha abiria waliolazimika kutafuta usafiri huo baada ya daladala  walizokuwa wamepanda kushindwa kuvuka eneo la Kawe-darajani, barabara ya Bagamoyo, kufuatia sehemu ya barabara hiyo kuharibiwa na mafuriko katika eneo hilo, jana.
 Wananchi wakisaidiana kunasua gari la mkazi wa Kawe-Darajani, baada ya gari hilo kuzolewa na mafuriko baada eneo hilo kukumbwa na mafuriko jana.
 Ofisi za Makao Makuu ya TLP zilizopo Magomeni Usalama, zikiwa zimekubwa na mafuriko.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages