DK. ASHA-ROSE ATAJA MAAZIMIO YA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM KILICHOFANYIKA DODOMA

Wednesday, May 22, 2013

DODOMA, Tanzania
Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, akizungumza na waandishi wa habari leo, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Amezungumzia kuhusu yaliyojiri kwenye kikao cha Kamati Kuu ya CCM, kilichofanyika jana, pia mjini Dodoma.

TAARIFA KAMILI KAMA ILIVYOTOLEWA NA DK. ASHA-ROSE

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ilifanya kikao chake cha kawaida mjini Dodoma Mei 21, 2013 chini ya Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Pamoja na mambo mengine Kamati Kuu ilijadili na kutafakari masuala mbali mbali yanayohusu Uchumi, Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Taifa.

MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI
Migogoro ya  wakulima na wafugaji imekuwa mingi na imeenea sana katika taifa letu. Migogoro hii inatokana na sababu nyingi: mabadiliko ya tabia nchi; ongezeko la idadi ya watu na mifugo. Kamati Kuu inasikitishwa na kuendelea kwa migogoro hii ambayo imekuwa tishio la amani na usalama katika jamii, na pia kusababisha wakulima kupata hasara baada ya mazao yao kuliwa na mifugo. Tumeishuhudia migogoro hii mkoani Morogoro hivi karibuni, katika ziara ya Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana na imeripotiwa katika maeneo mengine ya nchi yetu.

Kamati Kuu inaiagiza Serikali kuishughulikia na kuitafutia ufumbuzi wa kudumu migogoro hii. Kamati Kuu inaiagiza Serikali kuharakisha zoezi la kutenga maeneo kwa ajili ya wakulima na wafugaji na kujenga miundombinu ya malisho, maji, na majosho ili kuwezesha wafugaji kutohamahama na mifugo yao.

KULINDA HIFADHI
Kamati Kuu imezungumzia suala la mahusiano kati ya Hifadhi za taifa, wafugaji na wananchi waishio katika vijiji vinavyozunguka Hifadhi hizo. Kamati Kuu inatambua umuhimu wa Hifadhi kwa manufaa ya taifa letu na vizazi vijavyo. Inasisitiza msimamo wake wa kuzilinda Hifadhi za taifa sanjari na kuanzisha na kuendeleza mahusiano hayo.

Kamati Kuu inaiagiza Serikali kuwashirikisha wananchi katika kutenga maeneo ya Hifadhi, kulinda maeneo ya wanyama pori na kutenga maeneo ya malisho ili kuondosha migogoro isiyo ya lazima katika maeneo yanayozunguka Hifadhi.

ZAO LA KOROSHO
Kamati Kuu ilijadili matatizo yanayolikabili zao la korosho ambayo ni: kuyumba kwa bei ya korosho, malipo ya wakulima kuchelewa, tozo nyingi wanazolipishwa wakulima na udhaifu wa baadhi ya vyama vya ushirika.
Tatizo hili limedumu kwa muda mrefu na linastahili kushughulikiwa kwa njia ya kipekee.

Kwa kutambua kwamba wapo  baadhi  ya viongozi  na watendaji wa Serikali, viongozi wa vyama vya ushirika na  wafanyabiashara binafsi wanaochangia  katika kuendeleza matatizo yanayowakabili wakulima  wa korosho:

Kamati Kuu inatamka kwamba hali hii haivumiliki. Kamati Kuu inaitaka Serikali kukaa na wadau wote na kuchukua hatua zitakazotoa ufumbuzi wa kudumu wa matatizo haya kwa zao la korosho. Kamati Kuu pia inaitaka Serikali kuwachukulia hatua za kisheria  hao wote wanaochangia kuendelea kwa matatizo haya  kwa wakulima wa korosho.

MIGOGORO YA KIDINI
Kamati Kuu imepokea taarifa ya namna migogoro ya kidini inavyoshughulikiwa na hatua zinazochukuliwa. Kamati Kuu inaipongeza Serikali na vyombo vya dola kwa namna inavyoendelea kukabiliana na wahalifu wanaotumia mgongo wa dini kuanzisha vurugu na uvunjifu wa amani katika nchi yetu. Kamati Kuu inatoa mwito kwa Watanzania kukataa vitendo vyote vinavyochochea migogoro ya kidini; wananchi wajihadhari na watu waovu wenye nia mbaya ya kuligawa taifa letu.

Pamoja na jitihada za vyombo vya dola hadi sasa, Kamati Kuu inaitaka Serikali iandae mkakati wa kuzuia migogoro ya kidini kabla haijajitokeza.

MAKAMPUNI NA VIWANDA VILIVYOBINAFSISHWA
Kamati Kuu imetafakari hali ya viwanda hivi. Ni muongo mmoja umepita tangu ubinafsishaji ulipokamilika. Kuuzwa kwa mashirika na viwanda vya umma kwa watu na makampuni binafsi kumekuwa na matokeo ya aina mbili:  yako yale yaliyobinafsishwa na yakawa  na maendeleo mazuri na kuchangia uchumi wa Taifa. Na
yako ambayo yanaendeshwa kwa kiwango cha chini au yamefungwa.

Kamati  Kuu inasikitishwa na hali hii, kwani viwanda vilivyofungwa ni vile vilivyokuwa vikifanya kazi muhimu ya uzalishaji.

Viwanda hivi ni vya korosho, usindikaji wa pamba, mafuta ya kula, viwanda vya mazao ya ngozi, na vinginevyo. Hali hii inalikosesha Taifa fursa za ajira, kukua kwa mapato, kuimarika kwa uzalishaji na kuongezeka kwa uuzaji wa bidhaa zilizosindikwa na kuzalishwa nchini.

Imedhihirika kuwa wafanyabiashara waliochukua viwanda hivyo ndiyo hao hao wanaofanya biashara ya kununua mazao ya kilimo na mifugo na kuuza nje kama bidhaa ghafi, wakati huo huo wakiwa wamevifunga viwanda hivi.

Kamati Kuu inaiagiza Serikali kufanya tathmini ya viwanda vilivyobinafsishwa ili kuvitambua vile vilivyofungwa, na kuwataka waliouziwa wavifungue na iwapo watashindwa kutimiza masharti yaliyowekwa, Serikali iandae utaratibu wa kuwapa watu wenye uwezo wa kuviendesha.

WAKULIMA WADOGO WA MIWA -
Kumekuwapo na migogoro ya muda mrefu kati ya wakulima wadogo wa miwa na Kiwanda cha Sukari cha Mtibwa mkoani Morogoro. Matatizo haya yameshughulikiwa na watendaji mbalimbali bila ya kupatikana kwa ufumbuzi wa kudumu.

Kamati Kuu inaiagiza Serikali kuushughulikia mgogoro huu na kuyapatia ufumbuzi wa kudumu matatizo ya wakulima wadogo wa miwa haraka iwezekanavyo.

PEMBEJEO ZA KILIMO
Chama kimejiridhisha kuwa suala la utoaji wa pembejeo za kilimo ni zuri na lenye mafanikio. Hata hivyo Kamati Kuu imepokea taarifa kuhusu matatizo yanayohusiana na usambazaji wa mbolea ya ruzuku.
Kwa baadhi ya maeneo mbolea ya ruzuku imekuwa ikitolewa kwa watu wasiohusika na wakati mwingine walanguzi wamekuwa wakiingilia kati ili kujinufaisha nayo.
Kamati Kuu inaiagiza Serikali kusimamia kwa umakini na kutafuta utaratibu bora zaidi na wenye tija wa kuwafikishia wakulima mbolea, kwa wakati na kwa uhakika.

MRADI WA UJENZI WA NYUMBA ZA WATUMISHI
 Kamati Kuu  imepokea taarifa na kuipongeza Serikali  kwa kutayarisha mpango kabambe wa ujenzi wa nyumba za watumishi wake. Mpango huu utatoa fursa kwa wafanyakazi ya kupata mikopo yenye masharti nafuu na hivyo kuwawezesha kuwa na makaazi yenye uhakika.

MWISHO: 
Kamati Kuu imeitaka Serikali  kuwasilisha utekelezaji wa maagizo haya mara kwa mara.

IMETOLEWA NA:
Asha-Rose Migiro, 
Katibu WA NEC – Siasa Na Uhusiano wa Kimataifa,
Mei 22, Dodoma.

KINANA KUMBURUZA MAHAKAMANI MBUNGE PETER MSIGWA


DODOMA, Tanzania
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, amempa siku 21, mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (pichani) kuomba radhi kwa madai yake kwamba kiongozi huyo (Kinana) amehusika katika usafirishaji wa pembe za ndovu, vinginevyo atamburuza mahakamani.

Kufuatia dhamira hiyo, Wakili wa Kinana, Eric S. Ng'maryo kwenda kwa Msigwa.

Kwa mujibu wa barua hiyo ya Mei 14, 2013, ambayo Nkoromo Blog imepata nakala yake, tuhuma hizo dhidi ya Kinana kutoka kwa Mbunge huyo ni za uongo na zenye kumkashifu, kumfedhehesha na kumshushia hadhi.

Barua hiyo inaeleza kwamba Msigwa alitoa matamshi hayo mchana wa Aprili 21, 2013 katika mkutano wa hadhara wa kisiasa uliofanyika Uwanja wa Shule ya Msingi Mbugani, Wilayani Nyamagana jijini Mwanza.

Barua hiyo inanukuu maneno ya Msingwa akisema "...Kinana meli zake ndizo zinahusika na kubeba mape,mbe nchi hii, Kwa siku katika nchi hii tembo 67 wanauawa."

Barua hiyo inazidi kumueleza Msigwa kwamba; "Umeshatamka maneno haya au, yanayofanana na haya, katika hotuba zako nyingine nje ya Bunge, katika hotuba hizo na ile ya Mwanza, uliahidi kuzungumza zaidi uwapo bungeni:

"Nia ya ahadi hiyo ilukuwa kunoa hamu ya umma kufuatilia zaidi tuhuma zako dhidi ya Ndugu Kinana na pia kujaribu kujificha kwenye kivuli cha kinga ya  Bunge; mambo yote mawili yakiwa ni matumizi maovu na mabovu ya nafasi yako ya kisiasa na ya ubunge.

IFUTAYO NI BARUA YA WAKILI WA KINANA KWENDA KWA MSIGWA




MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MKUTANO WA 14 WA BARAZA LA USIMAMIZI WA MAWASILIANO AFRIKA, JIJINI DAR LEO

Tuesday, May 21, 2013


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akifungua rasmi Mkutano wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa leo Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam. Picha na OMR 
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo kutoka nchi za Afrika, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akifungua rasmi mkutano huo wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa leo Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam 
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo kutoka nchi za Afrika, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akifungua rasmi mkutano huo wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa leo Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam 
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo kutoka nchi za Afrika, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akifungua rasmi mkutano huo wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa leo Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongoza na Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Prof. John Mkoma, wakati akiondoka kwenye chumba cha mkutano baada ya kufungu rasmi mkutano huo wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa leo Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na baadhi ya washiriki wa mkutano huo.


Na Mwandishi Wetu


MAKAMU wa Rais Tanzania Bara, Dk. Mohammed Gharib Bilal, ameitaka sekta ya mawasiliano nchini kuhakikisha inakomboa wananchi kiuchumi, afya,kilimo na kielimu.

Bilal alisema kuwa huduma za kibenki na kutuma fedha zitasaidia kuondoa daraja lililokuwepo kati ya vijiji na mijini kutoka na huduma hizo kutumia mtandao ya simu.

Akizungumza leo katika ufunguzi wa mkutano wa 14 wa baraza la mawasiliano Afrika Dk. Bilal, alisema kuwa Serikali itahakikisha inatoa afya bora, maji salama ya kunywa na usafi wa mazingira, elimu, chakula na malazi,

Pia alisema kuwa itahakikisha inaboresha afya ya uzazi na kupunguza vifo vya watoto wachanga, kuwawezesha wanawake na wananchi wenye mazingira magumu zaidi ya jamii na kuhakikisha kunakuwepo na mazingira endelevu.

Dk. Bilal alisema mawasiliano ya makampuni katika Afrika yakifanya kazi kwa pamoja yatasaidia kuinua watu waishio vijijini na kutoa huduma bora ikiwemo kurahisisha upatikanaji wa mawasiliano na huduma za mtandao.

Mkutano huo umeandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), na kuhudhuriwa na waziri wa Mawasiliano na Teknolojia, Prof Makame Mbarawa na Mawaziri wa mawasiliano kutoka Sudan na Ghana.

KATUNI YA LEO


RAIS KIKWETE AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM, DODOMA LEO

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimkaribisha Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kufungua na kuendesha kikao cha Kamati Kuu ya CCM, leo katika ukumbi wa Jengo la White House mjini Dodoma. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar), Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Sheni na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar), Philip Mangula.
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiendesha kikao hicho cha Kamati Kuu ya CCM, leo mjini Dodoma.
Taswira kwenye kikao hicho cha Kamati Kuu ya CCM.

TANGAZO: MJADALA WA KISIASA UK


NAPE: WALIOANDIKA GAZETINI KUWA JK AMERUHUSU WATAKA URAIS KUJIPISHA PITISHA WAONGO

* ASEMA WAMEUDANGANYA UMMA KUKIDHI AJENDA YAO YA SIRI
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye amekanusha vikali habari zilizoandikwa kwenye baadhi ya magazeti kuwa Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete, ameruhusu wanachama wanaotaka Urais  kwa tiketi ya CCM, 2015,  kupitapita kwa kwa wanachama pamoja na kumjaza sifa mmoja wa wana CCM anayedaiwa kutaka kuwania urais 2015.

Alifafanua kuwa yeyote anayethubutu kufanya hivyo anakiuka kanuni za chama hicho na akibainika atachukuliwa hatua kali za kinidhamu ikiwemo kufungiwa kugombea uongozi katika chama na dola.
Baadhi wandishi wa habari wakiwa kwenye mkutano huo.
IFUATAYO NI TAARIFA KAMILI KAMA ILIVYOTOLEWA NA NAPE
TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI

Mei 19, 2013 Chama Cha Mapinduzi kilifanya kikao cha siku moja na wabunge wanaotokana na CCM, kikao hicho kilifanyika mjini Dodoma ambapo pamoja na viongozi wengine wa juu wa CCM kikao hicho kilihudhuriwa pia na Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete.

Kikao hicho kilikuwa na lengo la wabunge wa CCM na viongozi wa CCM wakiongozwa na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM ambaye pia ni Rais na
mtekelezaji mkuu wa Ilani ya uchaguzi ya CCM kubadilishana uzoefu wa namna ilani ilivyotekelezwa hasa kwenye majimbo kwa kipindi cha nusu ya muhula wa miaka mitano. Baada ya kubadilishana mawazo uliwekwa mwelekeo wa namna bora ya kutekeleza ilani na ahadi mbalimbali kwa kipindi kilichobaki.

Kwahiyo kwa kifupi lengo la kikao hicho ilikuwa ni kutathimini utekelezaji wa ilani majimboni na kuangalia namna bora ya kuweka msukumo mpya
na mkubwa zaidi kwa kipindi kilichobaki cha utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM kwa 2010/2015, lengo likiwa kuhakikisha ilani na ahadi za CCM na wagombea wake zinatekelezwa kwa kiwango kikubwa.

Hata hivyo baada ya semina hiyo baadhi ya vyombo vya habari vimenukuu kauli inayodaiwa kutolewa na Mwenyekiti wa CCM Dr. Jakaya Kikwete kuwa ameruhusu wanaokusudia kuomba ridhaa ya CCM kugombea Urais wa 2015 kufanya kampeni.

CCM imesikitishwa na nukuu hiyo ya kupotosha ukweli wa kilichojadiliwa na hivyo tumelazimika kutoa ukweli wa kilichojiri na kujadiliwa. Ni kweli kuwa mjadala juu ya watu mbalimbali wanaotajwa au wanaojitaja kuwa na nia ya kugombea nafasi mbalimbali hasa udiwani, ubunge na Urais ulikuwepo na ulikuwa mkali.

Hata hivyo hitimisho la kikao na majumuisho ya Mwenyekiti wa CCM Taifa lilikuwa ni kukemea kwa nguvu zote pirika hizo na uvunjifu huu wa makusudi wa kanuni za Chama chetu ambazo kimsingi pirika hizi zinakigawa Chama na kuvuruga mshikamano na umoja ndani ya Chama.

Nasisitiza nukuu hiyo ya baadhi ya vyombo vya habari si sahihi na ni ya kupotosha ukweli. Inaelekea kuna kikundi cha watu wanamgombea
wao wa kuchonga ambaye bila shaka anapungukiwa na sifa, hivyo wanajaribu kumuongezea sifa kwa kumlisha Mwenyekiti maneno na kuwaapa baadhi ya waandishi, uhuni huo haukubaliki.

CCM ina kanuni na taratibu zake zinazoisimamia na kuiongozakatika kufanya shughuli zake mbalimbali zikiwemo za mchakato wa kuwapata wagombea
wake katika ngazi mbalimbali kuanzia shina hadi taifa.

Kanuni hizo ni pamoja na kanuni za Uteuzi wa wagombea wa CCM kuingia katika vyombo vya dola toleo la Februari, 2010 na Kanuni za uchaguzi wa CCM, toleo la 2012.

Katika Kanuni za Uchaguzi wa CCM Toleo la 2012 kanuni za jumla Ibara ya 33 inazungumzia Miiko ya kuzingatiwa wakati wa shughuli za uteuzi na uchaguzi. nanukuu“ Maadili na nidhamu ya chama katika kusimamia na kutekeleza shughuli za uchaguzi wa chama lazima kuzingatiwa na wale wote
wanaohusika. Hivyo yawapasa kuelewa na kutambua kuwa;-

(1). “….wanachama wenye nia ya kugombea hawaruhusiwi kufanya kampeni ya aina yoyote kabla ya majina yao kuteuliwa na kikao kinachohusika”.

(4). “Ni mwiko kwa kiongozi au mwanachama yeyote wa CCM kuunda vikundi visivyo rasmi ndani ya chama, au kushiriki katika kampeni za uchaguzi za chini chini kinyume na ratiba ya uchaguzi na taratibu rasmi zilizowekwa”.

Ibara hiyo ya 33 kifungu kidogo cha 1 na 4 vinaweka wazi msimamo wa kikanuni wa Chama. Hivyo basi kwa mujibu wa kanuni za Uteuzi wa wagombea wa CCM kuingia katika vyombo vya dola toleo la Februari, 2010 na Kanuni za uchaguzi wa CCM, toleo la 2012 na kwa mujibu wa maagizo yaliyotolewa na kupokelewa kwenye kikao cha Mwenyekiti wa CCM Taifa na wabunge wa CCM mjini Dodoma tarehe 19/05/2013;

Ni marufuku kwa mwanachama yeyote wa CCM anayetaka kuomba
CCM impe nafasi ya kugombea kwenye uchaguzi wa dola kujipitishapitisha na kuita wapiga kura na kukutana nao kinyume na kanuni za Chama. Hatua kali zitachukuliwa kwa mwana CCM yeyote atakaye kiuka agizo hili.

Lakini pia ni marufuku kwa viongozi na watendaji wa Chama
kujihusisha na kuwakusanyia wapiga kura watu hao wenye nia ya kugombea kupitia CCM kwenye uchaguzi wa dola. Hatua kali zitachukuliwa dhidi ya viongozi na watendaji wote watakao kiuka agizo hili la Chama.


Tunawataka wote wenye nia, viongozi na watendaji wa CCM
kuzingatia agizo hili, ili tusije laumiana mbele ya safari.
Imetolewa na;-

Nape Moses Nnauye
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi

RAIS KIKWETE AONGOZA MAMIA YA WAOMBOLEZAJI KATIKA MAZISHI YA MZEE ALLY KLEIST SYKES

Monday, May 20, 2013

  Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali, Rais wastaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi na Mzee Benjamin William Mkapa, Waziri Mkuu Mstaafu Dkt Salim Ahmed Salim, Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kianana wakiungana na mamia ya waombolezaji katika mazishi ya Mzee Ally Kleist Sykes, mmoja wa waasisi wa chama cha TANU, leo katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam leo Mei 20, 2013
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete, akitia udongo kwenye kaburi wakati wa mazishi ya Mzee Ally Kleist Sykes, mmoja wa waasisi wa chama cha TANU, leo katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam leo Mei 20, 2013. Picha na Ikulu

WANAOCHAFUA KINYWAJI CHA KIROBA WASHITAKIWA BARAZA LA HABARI TANZANIA (MCT)


ALLY SYKES KLEIST AFARIKI DUNIA NCHINI KENYA LEO

Sunday, May 19, 2013


MWENYEKITI WA CCM RAIS KIKWETE AFANYA KIKAO NA WABUNGE WA CCM, LEO MJINI DODOMA

 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwasili ukumbini wakati wa kikao chake na wabunge wa CCM, leo Mei 19, 2013, katika ukumbi wa jengo la White House, Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma. Wengine kushoto ni Spika wa Bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama na Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akizungumza wakati wa kikao chake na wabunge wa CCM, leo Mei 19, 2013, katika ukumbi wa jengo la White House, Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma. Wengine kushoto ni Spika wa Bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama na Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula.
  Wabunge wa CCM wakiwa kwenye kikao chao na Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete leo kwenye ukumbi wa Jengo la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.
 Wajumbe kwenye kikao hicho wakibadilishana mawazo ukumbini. Walioketi mbele, Kushoto ni Katibu wa NEC Uchumi na Fedha Zakiah Meghji na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na kulia ni Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migoiro na Mbunge wa Urambo na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta.
  Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Mwigulu Nchemba akibadilishana mawazo na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanzibar) Vuai Ali Vuai na Katibu wa NEC Oganaizesheni Dk. Muhammed Seif Khatib kwenye kikao hicho.
 Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro(kulia) akisalimiana na Mbunge wa Viti Maalum Vicky Kamata wakati wa kikao hicho. Kushoto ni Mbunge wa Same Anne Kilango Malecela.
 Mbunge wa Songea na Waziri wa Mambo ya Ndani,Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akitaniana kuhusu Uyanga na Simba na Mwenyekiti wa Simba, Mbunge wa Tabora Aden Rage nje ya ukumbi kabla ya kuanza mkutano huo. Kulia ni Mbunge wa Viti Maalum Esther Bulaya.
Mbunge wa Bunga Steven Wasira (kulia) akibadulishana mawazo na wabunge wenzake, Dk. Kamani na Mkullo kabla ya kikao kuanza
Mbunge wa Kinondoni, Iddi Azan (kushoto) akibadilishana mawazo na wabunge wenzake Khamis Kagasheki na Shabiby nje ya ukumbi
Wabunge wakifurahia jambo nje ya ukumbi wakati wa mkutano huo, Kutoka kushoto ni Dk. Mary Mwanjelwa,  Ritha Kabati, Angela Kairuki, Beatrice Shelukindo na Vicky Kamata
Shabiby akizungumza na Angela Kairuki
Vicky Kamata na Ana Kilango Malecela ukumbini
Dk. Asha-Rose Migiro akimsalimia Mama Anna Kilango Malecela
Dk Maua Daftari na Samiah Suluhu ukumbini
Job Ndugai akimpongeza Mbunge wa Igunga Dk. Dalaly Peter Kafumu kurejeshewa Ubunge
Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro akimsalimia Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa wakati wa kikao hicho cha Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete na wabunge wa CCM
Mbunge wa Kyela Dk. Harrison Mwakyembe akimsikiliza kwa makini Mbunge mwenzake Innocent Kalogeris  wakati wa mkutano huo. Picha zote na BASHIR NKOROMO

YANGA YATWAA UBINGWA KWA MARA YA 24, YAICHAPA SIMBA 2-0

Saturday, May 18, 2013

Beki wa Simba, Musa Mudde (kushoto) akichuana na mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, leo. 
Beki wa Simba, Shamte Ramadhani akimtoka mshambuliji wa Yanga, Simon Msuva
Nahodha wa Yanga, Nidir Haroub 'Canavaro' akiwa amenyanyua kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara pamoja na wachezaji wenzake.
Shabiki wa Yanga akipelekwa kupewa huduma ya kwanza baada ya kuzimia wakati mchezo ukiendelea.
Kikosi cha Simba.
Makocha wa yanga wakipanga mikakati ya Ushindi.
Timu zikiingia uwanjani.
Timu zikisalimiana.
Kocha wa Simba, Patrick Liewig
Kocha wa Yanga, Ernst Brandts
Beki wa Simba, Shomari Kapombe akimtoka mshambuliji wa Yanga, Simon Msuva
Msanii Juma Nature akitumbuiza wakati wa mchezo huo. 
Mshambuliaji wa Simba, Felix Sunzu akitafuta mbinu za kuwatoka mabeki wa Yanga. 
Mashabiki wa Yanga.
 Raha ya ushindi.
 Kocha wa Yanga, Ernst Brandts akiwa amebebwa na wachezaji wake.
 Kiduku
KARIBU JANGWANI NGASA
Mashabiki wa Yanga wakiwa wamembeba mshambuliaji
wa Simba, Mrisho Ngasa mara baada ya mpira kumalizika, ikiwa ni ishara ya
kumkaribisha katika klabu yao. 


Mashabiki wa yanga.
Wachezaji wa timu ya Yanga wakishangilia ubingwa
wa Ligi Kuu ya Vodacom baada ya kuifunga Simba 2-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa  jijini Dar es
Salaam
Kipa wa Simba, Juma Kaseja akijaribu bila
mafanikio kuokoa mpira wa kichwa uliopigwa na mshambuliaji wa Yanga, Didier
Kavumbagu katika mchezo wa kufunga pazia la Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


KARIBU NYUMBANI
Mashabiki wa Yanga wakiwa wamembeba mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngasa mara baada ya mpira kumalizika, ikiwa ni ishara ya kumkaribisha katika klabu yao. 

Refa wa mechi ya Simba na Yanga, Nartin Saanya akiwa chini baada ya kugongwa kwa bahati mbaya na mchezaji wa Yanga, Didir Kavumbagu.
Refa, Martin Saanya akipata matibabu.